Jumatatu, 23 Oktoba 2017

WALI NA MAHARANGE



KUPIKA MAHARAGE
Chambua maharage  yako vizuri,  yaoshe halafu weka kwenye  sufuria safi, weka maji kiasi kisha yachemshe mpaka yaive.
Yakishaiva ipua, chukua sufuria safi bandika jikoni likishakauka maji mimina mafuta ya kula yaache yapate moto.
Baada ya hapo weka vitunguu maji ambavyo umevikatakata vipande vidogovidogo, kaanga mpaka vibadilike rangi na kuwa vya kahawia (brown), weka karoti ambazo umekata vipande vidogovidogo.
Vikishaiva weka maharage uliyochemsha na chumvi kiasi, vikishachanganyikana weka tui la nazi subiri lichemke kwa dakika tano na hapo mboga yako itakuwa tayari.
WALI WA ILIKI
Pepeta mchele wako vizuri ili kutoa uchafu.
Chukua sufuria safi, weka maji yanayotosha kupika wali wako kisha yabandike jikoni huku ukiweka chumvi, mafuta ya kupikia na iliki halafu funika.
Yaache yachemke, baada ya hapo weka mchele ambao tayari umeshauosha kisha koroga huku ukiangalia kama                    chumvi imekolea.
Baada ya hapo funika subiri maji yakikaukia geuza ili uive pande zote.
Funika kisha subiri kwa dakika kadhaa geuza tena kwa mara ya pili ukiona maji yamekauka kabisa, hapo wali wako utakuwa tayari kwa kula.


MAANDALIZI YA KUPIKA CHAPATI ZA MAJI



Jinsi ya kupika Chapati za maji: Leo ninakuletea hatua kwa hatua namna ya kuandaa na kupika Chapati laini za Mayai. Tafadhali fuatana nami katika pishi hili.
Pishi: Chapati za maji/laini
Utangulizi: chapati ni kitafunwa au chakula kinachopendwa na wengi. Kuna Chapati za Kusukuma na Laini au za maji. Aina hii ya pili hupendwa zaidi na watu kwa sababu ni rahisi kutayarisha. Fuatana nami hatua kwa hatua namna ya kuandaa pishi hili tamu
Mahitaji
  • Ngano 1/2 kilo
  • mayai 3
  • mafuta au samli 1/4 kikombe
  • kitunguu kikubwa kilichosagwa 1
  • Kitunguu Swaumu punje 4
  • Chumvi 1/2kijiko au kulingana na matakwa yako
Mahitaji
Namna ya kupika chapati za maji
  1. Chekecha unga wako vizuri weka katika bakuli safi.
  2. Tia maji katika bakuli la unga na ukoroge mpaka upate uji wa wastani si mzito san a wala si mwepesi sana.
  3. Ongeza mayai na chunmvi endelea kukoroga.
  4. Ongeza kitunguu swaumu na kitunguu maji. Injika kikaango chako jikoni subiri kipate moto.
  5. Chota pawa moja mimina na tandaza kuzunguka kikaango subiri sekunde tano hadi kumi mpaka ikauke kisha geuza upande wa pili.
  6. Tia mafuta huku ukigeuza na kuzungusha ili mafuta yaenee pande zote na ili chapati isiungue. Endelea kugeuza mpaka iwe rangi ya kahawia.
  7. Hapo chapati zitakua tayari kwa kuliwa.
  8. Fanya hivyo kwa chapati zote zilizobakia
Matayarisho hayo yanatosha kupika chapati za mayai/laini sita (6) mpaka kumi (10) . Chapati za maji hupendeza zaidi kuliwa Michuzi mizito, Chai na kadhalika. Nenda kajaribu kuandaa pishi hili kisha uje utupe mrejesho. Kama una maoni yoyote kuhusu Jinsi ya kupika chapati za Maji na Mayai andika hapo chini. Asante


JINSI YA KUPIKA WALI NA NGEGERE



Tangu nilipokuwa mdogo ilikuwa siku wakipika njegere na tukala na wali kusema kweli nilikuwa nafurahi kiwango kikubwa sana. Zaidi pale inapokuwa njegere zimeungwa na tuzi zito la nazi. Sasa nishakuwa mtu mzima na najua kupika hivyo mara nyingi huwa najipikia.
Hili ni pishi moja rahisi sana kwa yeyote anaweza pika bila kukosea. Mahitaji ya kawaida tu ni njegere, nazi, vitunguu , nyaya ila sasa kuna ziada ili kuongeza nakshi nakshi na ndio mimi sasa leo nakuelekeza vile ambavyo mimi huwa napika
MAHITAJI
  • Glass 3 za njegere
  • Vitunguu maji viwili – vikatwekatwe
  • Nyanya 3 – Zimenywe na kukatwa katwa
  • Karoti moja – Ikatwe vipande vidogo dogo
  • Mchanganyiko wa Kitunguu swaumu na Tangawizi kijiko 1 cha chai
  • Mahanjumati masala kijiko 1 cha chai – Waweza tumia spice mix aina yoyote ikiwa hauna Mahanjumati masala
  • Tui zito la nazi Glass moja 1
  • Mafuta ya kula vijiko 3 vya mezani
JINSI YA KUPIKA
  1. Kwanza chemsha njegere zako hadi kuiva ila sio kurojeka – zikiwa tayari weka kando
  2. Weka chombo unachotumia kuunga mboga na uweke mafuta yakiaanza kupata moto weka vitunguu maji na endelea kukaanga hadi vilainike
  3. Vikiisha kulainika weka ule mchanganyiko wa kitunguu swaumu na tangawizi. Endelea kuvipika vikiwa kama vinaanza kubadiri rangi sasa weka zile nyanya.
  4. Zipike nyanya hadi zitakapoiva na kuwa kama zinatengana na mafuta ndipo unaweka karoti na mahanjumati masala au spice mix ulionayo kwa sekunde chache kisha unaweka njegere
  5. Ili zisiwe kavu sana unaweza ongeza kidogo yale maji yaliyotumika kuchemsha njegere. Ongeza na chumvi kiasi upendacho. Kisha mchanganyiko huo uendelee kuchemka kwa dakika 3-4
  6. Sasa weka lile tui la nazi na punguza moto. Baada ya kuweka tui la nazi endelea kukoroga kwa dakika chache hadi itakapoanza kuchemka taratibu. Baada ya hapo epua na tayari kwa kula.
Furahia pishi hili zuri la Njegere Nazi. Hapa chini nimeweka video nikionyesha jinsi ya kukuna nazi na kutengeneza tui la nazi.





JIFUNZE JINSI YA KUPIKA BAGIA ZA DENGU



Mapishi ya Bagia dengu
Mahitaji
Unga wa dengu (gram flour 1/4 kilo)
Kitunguu kilichokatwa (onion 2)
Hoho (green pepper 1/2)
Pilipili iliokatwakatwa (scotch bonnet pepper 1/2)
Barking powder (1/4 ya kijiko cha chai)
Chumvi (salt)
Kitunguu swaum (garlic cloves 2)
Mafuta ya kukaangia (vegetable oil)
Binzari manjano (turmeric 1/4 ya kijiko cha chai)

Matayarisho
Changanya unga, chumvi, binzari, barking powder kwanza kisha weka maji kiasi na vitu vyote vilivyobakia (isipokuwa mafuta) na ukoroge vizuri kuhakikisha unga hauna madonge.

Hakikisha unga hauwi mzito wala mwepesi sana. Kisha uache kwa muda wa dakika 20. Baada ya hapo choma bagia katika mafuta. Ukiwa unachoma hakikisha bagia zinakuja juu ya mafuta na hazigandi chini.

Ikitokea zinaganda chini hapo itakuwa umekosea kitu. Pika mpaka ziwe za light brown kisha zitowe na uziweke katika kitchen towel ili zikauke mafuta na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Karibuni!!